UKATILI!! MWANAUME AMNYWESHA MPENZI WAKE TINDIKALI, KISA WIVU.....



Jitendra Sakhpal akisindikizwa na polisi kuingia mahakamani. Msichana mdogo ameungua vibaya baada ya rafiki yake wa kiume aliyevunja naye uchumba kudaiwa kumtega walipokutana, kumlazimisha kunywa tindikali na kumsukumia kwenye bahari.

Ripoti nchini India zinadai msichana huyo hapo kabla alikuwa mpenzi wa Jitendra Sakhpal, miaka 21, ambaye alikuwa amemchumbia, lakini alikataa kuolewa naye na kusitisha mahusiano hayo sababu familia yake haikumridhia mwanaume huyo asiye na ajira.
Baba wa msichana huyo aliripotiwa kuieleza polisi kwamba mvulana huyo alikuwa akiwasumbua, na ndugu mmoja wa kike alidai kwamba Sakhpal alitishia kumuua baba wa msichana huyo, kwa mujibu wa ripoti hizo.
Msichana huyo, ambaye hakutajwa jina, anaripotiwa kuwa mahututi kwenye Hospitali ya Thunga, mjini Mumbai.
Sakhpal amekamatwa na kushitakiwa kwa jaribio la mauaji.
Shambulio hilo limetokea Jumamosi huko Gorai Beach katika kitongoji cha magharibi mwa Mumbai. Wote ni wakazi wa Dahisar mjini Mumbai.
Msichana huyo mwenye miaka 18, mwanafunzi wa HSC ambaye ametokea Borivali, alikutana na Sakhpal wakati akiondoka chuoni Jumamosi, kwa mujibu wa Polisi.
"Jumamosi, Sakhpal alikutana na msichana huyo nje ya chuoni kwake huko Gorai na kumtaka amsindikize kwa matembezi kidogo. Wawili hao walipanda boti na kwenda kijiji cha Gorai," inspekta wa ngazi ya juu Deepak Bagawe alieleza.
Inspekta huyo alisema Sakhpal alijaribu kumshawishi mpenzi wake huyo wa zamani kurejesha mahusiano yao, lakini pale binti huyo alipokataa alidaiwa kutoa tindikali hiyo.
Kwa mujibu wa polisi, alidaiwa kumpanua msichana huyo mdomo na kujaribu kumimina tindikali hiyo ndani ya mdomo wake. Kiasi kidogo kilimwagikia usoni mwa binti huyo na kupata majeraha ya kuungua kwa asilimia 10-15.
Madaktari sasa wanajaribu kutathmini kiasi gani cha madhara ya ndani ya mwili aliyopata.
"Sakhpal anaonekana kuwa alipanga hayo kabla kutokana na kuwa amebeba kabisa tindikali hiyo," msaidizi wa kamishna wa polisi Mahesh Patil, alieleza.
Taarifa zinasema kwamba baada ya baba wa msichana huyo kulalamika kwa polisi kuhusu mvulana huyo, wawili hao waliripoti kwenye kituo cha polisi na 'kuandika kwamba hawatakutana tena na suala hilo limeshapatiwa ufumbuzi," alisema Deepak Bagawe, inspekta wa ngazi ya juu wa polisi wa Gorai.
Mmoja wa jamaa wa binti huyo alieleza: "Hapo awali tulifungua madai kuhusu kijana huyo. Alizoea kumtesa binti huyo na kumpiga hadharani. Alifikia hata kumtishia kumuua yeye na baba yake."
Hali ya binti huyo inaimarika lakini bado hawezi kutoa maelezo, kwa mujibu wa polisi walionukuliwa.
Ripoti zimedokeza kwamba baba wa msichana huyo anafanya kazi kwenye halmashauri ya mji huo wakati baba wa mvulana huyo ameajiriwa na kampuni binafsi

No comments:

Post a Comment