Mhariri wa Gazeti la Ijumaa Wikienda, Sifael Paul (kushoto) akiwa na Mhariri Msaidizi wa Magazeti ya Risasi na Amani, Erick Evarist msibani hapo.
Baba Mzazi wa Prof Jay, Mzee Haule (kushoto) akibadilishana mawazo na mzee mwenzake msibani hapo.
Nature (kushoto) na Dolo wakiwa msibani.
Waombolezaji wakipata menyu.
Watu mbalimbali wamezidi kumiminika nyumbani kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Joseph Haule ‘Prof. Jay’ eneo la Mbezi Mwisho jijini Dar kutoa pole kufuatia kifo cha mama yake mzazi Rosemary Majanjala. Marehemu Rosemary aligongwa na gari aina ya Stallet juzi saa mbili usiku ambapo alifariki baada ya kufikishwa katika hospitali ya Tumbi iliyopo Kibaha, mkoani Pwani.
No comments:
Post a Comment