Matiko Joseph mmoja wa waathirika waliokunywa dawa akiwa amelazwa hospitali. Picha na Antony Mayunga. |
Mwalimu aliyetumia uchawi kuwaroga wezi, amejikuta akiwaroga shemeji zake waliopata uchizi
hakuweza kuvamiwa na wezi hao, lakini mke mkubwa alipigwa hadi kulazimika kupewa matibabu hospitali.
Butiama. Ilikuwa kama simulizi ya
kwenye filamu, baada ya mganga wa kienyeji aliyeletwa toka Kenya kuja
kuwaroga wezi walioiba nyumbani kwa Mwalimu mstaafu, Raphael Omwando
(60), baada ya dawa yake kuwatia uchizi ndugu wa mke mkubwa wa
aliyeibiwa.
Mwalimu Omwando ambaye ana wake wawili alivamiwa
na wezi waliomwibia pikipiki na mali nyingine, ikiwemo kumjeruhi yeye
(Omwando) na mkewe mkubwa. Mke mdogo aliyemuoa hivi karibuni anaishi
kwenye nyumba nyingine nahakuweza kuvamiwa na wezi hao, lakini mke mkubwa alipigwa hadi kulazimika kupewa matibabu hospitali.
Watu walio karibu na familia hiyo walisema
kutokuelewana kati ya mke mkubwa na mdogo, kulimfanya mke mkubwa
aliyejeruhiwa na majambazi kumtuhumu mke mdogo kwamba alishirikiana na
majambazi hao.
Filamu hiyo ya familia ilianza kwa ndugu wa mume
(Omwando) wanaoishi Kenya, kuleta sangoma kwa ajili ya kubaini wezi
waliomwibia ndugu yao.
“Sijui nimefikaje hapa hospitali…maana kumbukumbu
zinaishia pale nilipolazimishwa kunywa dawa na mganga wa kienyeji
(Sangoma) anayedaiwa kutokea nchini Kenya …ili wezi wa pikipiki na vifaa
vya mwalimu mstaafu virudishwe,” hiyo ni kauli ya mmoja kati ya watu
wanne waliolazwa hospitali kwa madai ya kurukwa na akili.
Wagonjwa hao ni vijana wanne wa Kijiji cha Kirumi Kata ya
Bukanga, Tarafa ya Makongoro, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara waliolazwa
hospitali ya Mkoa wa Mara baada ya kunywa dawa hiyo na kupoteza fahamu
huku wakionekana kama mazuzu (Mazombi).
Waathirika
Matiko Joseph (25) anasema yeye alilazimishwa
kunywa dawa nyingi pamoja na makapi yake,” …Baada ya kumtajia mganga
hivyo akasema ninyi kunyweni nyingi…dawa ilikuwa na ukakasi
ilinikereketa sana. Baada ya kunywa niliondoka lakini baadaye hali
ikabadilika sana,” anasema na kuongeza,
“Nilishtukia niko hospitali tayari ikiwa ni siku
ya pili …Nikisimuliwa ilivyokuwa nazidi kushangaa…huyo mganga alilenga
kutuua kabisa….maana wakati anatoa dawa alisema atakayepata madhara
hatapona hata akipelekwa wapi mpaka vitu virudi ama fedha…akaondoka
kwenda Kenya na hakuacha simu wala jina lake kujulikana,” anasema Joseph
huku akipumua kwa harakaharaka.
Tura Joseph (30) anasema wengine walikunywa kidogo
lakini wao wana ndugu walilazimishwa kunywa zaidi kwa kile kinachodaiwa
kuwa walihisiwa kula njama za kumdhuru shemeji yao, na ndiyo
walidhurika zaidi.
Anasema baada ya kunywa alihisi kitu kinamkaba
shingoni na kuishiwa nguvu, akawa hoi na kuanza kuongea maneno
yaliyowatia shaka, ndugu wakawabeba kwa bajaji hadi hospitali.
No comments:
Post a Comment