Ni imani yangu kwamba kupitia vyombo mbalimbali vya habari na
mitandao jamii,unafuatilia tukio zima la kusikitisha la kutekwa nyara
na kujeruhiwa vibaya kwa Dr.Steven Ulimboka hapo juzi. Kama bado
hujasikia au kufuatilia kwa kina,Gazeti La Mwananchi linayo taarifa ndefu na pana ambayo unaweza kuisoma kwa kubonyeza hapa.
Lakini wakati mtaani kukiwa na kila aina ya tetesi na
mazungumzo,kubwa zaidi ni kujua hali ya Dr.Ulimboka.Sote,bila shaka
tunamtakia uponaji wa haraka. Hizi hapa ni picha kutoka
alipolazwa(Muhimbili) ambazo zimetoka kwa Da Subi pale www.wavuti.com.
Naelewa kwamba zinasikitisha na pengine zisingefaa kuwepo katika
ukurasa wa mbele namna hii.Pamoja na hayo(na ninaomba radhi) zipo
nyakati ambapo mambo mengine lazima yawekwe hadharani kama
yalivyo.Zitazame na kisha tembelea www.wavuti.com uone video kidogo ikiwa na ujumbe kutoka kwa Dr.Ulimboka.